The Tech Planner

Featured post

USALAMA APP REVIEW

Its agreeable that worst things tend to happen to us when we are alone: Be it health emergencies,  crimes etc. .All these happen to us unex...

Friday 27 May 2016

POST YA NOTIFLOW INAYOZUZUA NA KUTESA INSTA +18 ONLY

Kwa Mara nyingine tena noti flow msanii kutoka Kenya ambaye amekua moja ya wasanii Wenye kuzua tashwishi miongoni mwa wakenya kwa mambo kadhaa anayofanya  zikiwemo hisia zake kuhusu ndoa ya jinsia moja,amerudi kwa vishindo!

Kwenye post yake latest ya insta ,  noti flow amewapagawisha mashabiki zake na kuwaacha wahuni vinywa wazi huku wakidondokwa na mate .

Itazame post yake kisha unipe comments hapa chini.

Share:

ZAWADI ALIYOPATA JULIANI

Juliani, star kutoka Kenya alizawadiwa kitabu, dakika kadhaa kabla ya kwenda mbele ya mashabiki zake kwenye "mic and dream concert"

Hakuhimili furaha yake na kuenda moja kwa moja hadi insta na kuandika

"Great surprise before the mic and dream concert, I got this book delivered. Written by Mwenda Ntarangwi,ASANTE sana Kimani Njogu for getting it to me"

Share:

SAUTISOL WALIVYOKICHANA NCHINI SOUTH AFRICA

Sauti Sol mastaa wa Africa kutoka nchini Kenya, Jana Mei 27, walitua nchini Afrika Kusini.
South Africa ni kati ya sehemu walizotembelea katika ziara yako maarufu ya "LIVE AND DIE IN AFRICA" ili kuipa msukumo album yao kwa jina hilo.

Tazama picha uone mambo yalivyokuwa Jana South Africa!

Share:

KING KAKA ATUA KISUMU!

Leo hii, jumamosi ya mei,28, Rabbit the king ,atatua katika mji wa kisumu kwa niaba ya kuwaburudisha mashabiki wake kwenye ziara kwa jina"THE KENYAN TOUR"

kwa watu wa eneo la Kisumu msikose,kwani Leo hii King Kaka atakua katika mji wenu,akiwatumbuiza "Rang'ala girls "



Comment hapa chini

Share:

DIAMOND PLATNUMZ TAKES BLINGS TO THE GRAM

Diamond platnumz ,hit maker mkubwa wa East Africa ,ambaye juzi tu amekua nominated kwenye BET AWARDS 2016,Katika kundi la best international act Africa,

Leo hii , amepeleka mashauzi moja kwa moja na kuonyesha kati ya  "blings" anazovaa za dhahabu na Almasi kwenye official yake ya insta @diamondplatnumz

Huenda ndiye the next king of bling in East Africa?

zitazame hapa


Au itazame video hapa 

 https://www.instagram.com/p/BF72et2mwJ-/

Share:

HUDDAH LANDS ANOTHER DEAL

baada ya kufanya kazi na  Vazzi clothing collection.' Huddah Monroe sasa amepata deal nyingine na hivi sasa ndiye brand ambassador wa BrightenMi Cosmetics katika sehemu hii ya Afrika mashariki.

”Meet our new #BrightenMi Ambassador for the East African region.#HONEY body and face cream are what she uses to eliminate blemishes and restore evenness,”waliandika kwenye post ya ya insta
hii ni mara ya pili  Huddah kuwa brand ambassador , baada ya kufanya kazi na ' Vazzi clothing collection.'
 
hongera Huddah!!
Share:

AUDIO ALERT! HARMONIZE FT KOREDEBELLO



inaonekana kuwa msanii Harmonize star wa bongo fleva ameachia kibao kipya huku akimshirikisha msanii mkubwa kutoka Nigeria Koredebello.Harmonize amejulikana kwa hits kama vile Aiyola na bado,kibao alichomshirikisha Diamond Platnumz.


katika post yake ya insta, Diamond platnumz ambaye ndiye mkubwa wa label ya WCB ameandika

Natamani Mngepata walau sekunde 3 tu kuskiliza Ngoma Mpya ya @Harmonize_tz alomshirikisha Mr Romantic, wenyewe wanamwita GODWIN @koredebello tokea the Marvins Nigeria.... Moja ya ngoma zinazotawala kwenye Repeat ya playlist yangu kwa sasa.... #BongoflavourTotheWorld

 

 

 

kaa kwenye blogspot ya Presenter Ali upate kujua punde audio ikitoka !!

Share:

Thursday 26 May 2016

AUDIO ALERT "DIVINE" BY PRIME

Kutana naye PRIME msanii kutoka nchini Kenya!
Jina halisi:Ochieng Eugene Omondi
Alipozaliwa:23 May ,Nairobi Kenya
Style ya nyimbo:Newlife RnB Pop Reggae Afrodancehalll
Ochieng Eugene Omondi alizaliwa May 23).Hapo Awali alijulikana kama Decimal ila alibadili jina na kujiita  PRIME mwaka huu wa 2016.
PRIME alianza safari yake ya muziki akiwa na miaka kumi na sita,kwa kibao kilichofanya vizuri kwa jina
"happy time" wimbo aliorekodi na wenzake katika bendi .
Baadaye, alitoka kwenye bendi hiyo na kuwa msanii anayeimba kivyake,ambapo aliachia hit single " Fine girl(irie)" iliyopokelewa vizuri ndani na nje ya East Africa.
Punde aliachia kibao " Jamming"
Baada ya kurebrand, PRIME sasa ameachia kibao "Divine"
Katika post yake ya insta :DIVINE
"Divine is a sexy simple chune for all ladies around the world regardless of race.Prime makes a very hot flow about  a lady with his powerful lyrics.He uses his one of a kind lyrical power and creativity to communicate.ladies buckle up."

click http://www.mdundo.com/a/14897 kuskiza na kudownload  wimbo wake mpya

  
Share:

Wednesday 25 May 2016

AUDIO ALERT! RAYMOND TIP TOP NATAFUTA KIKI

Baada ya hit single ya Raymond Tip Top,kwa jina #kwetu , Leo hii star huyu wa bongo fleva ameachia kibao kipya kwa jina #NATAFUTAKIKI

Unaeza kuiskiza na kudownload hapa

Share:

Friday 20 May 2016

MAYUNGA FT AKON "DON'T GO AWAY"

Mayunga,msanii kutoka nchini Tanzania,aliyeiwakilisha nchi hiyo kwenye Airtel Trace Music Star (sehemu ya kwanza mwka 2015),na kuibuka  mshindi, ameachia hit single mpya kwa jina "don't go away"

katika wimbo wake mpya, Mayunga amemshirikisha msanii maarufu star wa Afrika Akon.

Itazame Hapa

Share:

DIAMOND PLATNUMZ ACHAGULIWA KUSHIRIKI KWENYE BET AWARDS 2016

Tanzania imeamkia  habari zinazosisimua baada ya  Diamond Platnumz kuchaguliwa tena kushiriki kwenye tuzo za kituo maarufu cha TV Marekani kiitwacho BET.hii ni awamu nyingine  ambapo Platnumz  amekuwa nominated kwenye tuzo hizi na sasa hivi ni kwenye tuzo za BET Awards 2016.

Diamond  Platnumz ameshukuru kwa kuchaguliwa kuwania tuzo hizi chini ya kipengele cha Best international Act Africa .

Kwenye post yake ya insta, ‘Ningependa niwashukuru kwa Sapoti kubwa Manayozidi kunipa na niwajuze kuwa kijana wenu nimechaguli kuwania tunzo ya Msanii Bora wa Kimataifa toka Africa kwenye tunzo za BET #BETAwards America’ aliandika punde tu baada ya kufikiwa na habari hizo njema.

Orodha ya waliochaguliwa kuwania huko marekani imesisimua huku   Beyonce, Rihanna na Drake wakitangazwa kuongoza kwa kuwania tuzo zaidi ya moja.

Miongoni mwa wasanii wa Afrika waliochaguliwa kushiriki ambao ni wapinzani wa Diamond ni AKA,yemi alade,wizkid black coffee,mzvee na wasanii wengine.

Share:

Thursday 19 May 2016

ALIKIBA KWENYE MKATABA NA SONY MUSIC

Alikiba  ni Mwimbaji staa wa bongofleva .kuanzia 19,mei 2016 atakua chini ya mwavuli wa Sony Music
.sony music ni kampuni kubwa ya muziki inayofanya kazi na mastaa wa dunia kama vile Beyonce, John Legend na Chris Brown.
Mkataba huo utahakikisha  kumtengeneza Alikiba kweye kiwango cha juu zaidi kimuziki na kibiashara huku ukigharamia video na anaporekodi audio zake.
Muziki wa Alikiba utasambazwa na Sony Music kwenye masoko makubwa ya muziki yakiwemo ya Marekani, Ulaya na hata  Africa.

Davido pia alitia sahihi mkataba huu na Sony music hapo awali.mkataba huu unamuwezesha msanii kukutanishwa na waandishi wakubwa wa nyimbo duniani,pamoja na kumrahisishia msanii kufanya collabo na wasanii maarufu duniani.

Subscribe kwenye YouTube channel ya Presenter Ali. Update story zaidi

Share:

MSICHANA MWINGINE KATI YA WALIOTEKWA NYARA NA BOKO HARAMA APATIKANA

miaka miwili tangu zaidi ya wasichana  276 wa shule watekwe nyara na kupatikana kwa mmoja mnamo May 18 2016 ,msichana mwingine Serah Luka  amepatikana kaskazini mashariki mwa jimbo la Borno.

Mkuu wa jeshi la polisi Nigeria amethibitisha taarifa hizo . hii ni baada ya Amina Ali msichana wa kundi la Chibok girls kupatikana mnamo mei 18,2016

Rais wa Nigeria alimualika Amina Ali,pamoja na mamake mzazi,na mtoto wake aliyejifungua wakati akiwa mateka wa kundi la kigaidi la Boko Haram.
Amina alisimulia kuwa  kati ya wanafunzi wenzake, sita walipoteza maisha walipokua mateka.

Share:

Tuesday 17 May 2016

HARMONIZE NA WOLPER KWENYE MAPENZI!!!

Harmonize msanii mpya aliyesajiliwa kwenye label ya WCB na Diamond Platnumz huenda baada ya ustar akajiri pia na mapenzi ya mjini!

Star huyu wa singles mbili "Aiyola" na kibao "Bado" alichomshirikisha Diamond platnumz huenda akawa na uhusiano na star muigizaji wa Tanzania Jacky wolper.

Harmonize AKA mapenzi, ameyamwaga mapenzi kwa wolper kwenye insta page yake .

Hii ni licha ya wolper kuwa mapenzi wa kitambo wa Diamond Platnumz. ila mapenzi hayachagui!!!

Tazama picha

Share:

Sunday 15 May 2016

ALIKIBA AACHIA KIBAO KIPYA #AJE

Baada ya lupela ,unconditionally bae na vibao vyenye kutisha ,Alikiba  al maarufu Kingkiba ameachia kibao kipya kwa jina #AJE . itazame teaser ya video Hapa


Utakipata kwenye official YouTube yake kuanzia 19-05-2016 

Share:

DIAMOND PLATNUMZ ABADILISHA MUONEKANO WA NYUMBA YAO

Diamond platnumz ametia bidii kuibadilisha hali ya nyumba yao iliyopo Tandale.

Licha ya umaarufu, Diamond platnumz bado ameonyesha bidii katika kuijali familia yake.
Hii ni baada ya kuibomoa nyumba yao ya kitambo na kuijenga upya

Tazama picha ya nyumba ilivyo sasa tofauti na ilivyokuwa zamani

Share:

SHOW YA DIAMOND PLATNUMZ ILIVYOTISHA HUKO UDOM

Mnamo tarehe 12 mwezi mei, Diamond Platnumz AKA Chibu Dangote pamoja na mastaa wa Africa Mafikizolo walifika Dodoma kwa nia ya kuwafurahisha na kuburudisha  wanafunzi mjini.

Diamond Platnumz alitisha zaidi kwa mihemko kwa mashabiki zake .

Show hii iliandaliwa na Vodacom ya nchini Tanzania.
Diamond ndiye brand ambassador wa Vodacom nchini humo.

Tazama video ya diamond alivyowapagawisha wanafunzi kwenye stage
Hapa

Share:

Friday 6 May 2016

" NAMJUA " VIDEO YA SHETTA IMETOKA

Siku mbili tu baada ya audio iliyotisha bongo, Mamba katika uwanja wa utunzi ,Shetta ameachia video ya hit single yake mpya kwa jina NAMJUA.

Muda mfupi tu baada ya kuachia video hii, baba Qayla amemiminiwa sifa na mashabiki wake wa insta pamoja na subscribers wa YouTube kwa ukali wa video na utunzi wake wa kutajika katika wimbo wake.



Itazame video hapa uburudike pia, kwa wimbo wa shetta wa kwanza kuufanya mwenyewe katika historia!

Share:

Thursday 5 May 2016

AUDIO YA P UNIT "HOLD TIGHT" IMETOKA!!

Imekuwa ni muda sasa  hatujaskia wimbo kutoka kwa wasanii wa P UNIT -Frasha,buganya na bon-eye .
Miezi kadhaa iliyopita, fununu zilitamba kwenye mitandao kuwa kikundi hiki kilitengana na kila msanii kwenda kivyake na kuanza safari mpya za kusaka hela kwa muziki wa genge.

Ila kwa sasa,
Kikundi hiki cha P UNIT, kimeachia kibao kipya kwa jina "HOLD TIGHT"

Kibao hiki kimeshughulikiwa na producer wao wa tangu jadi, Decimal kwa jina maarufu Musyoka.

Je huenda kibao kibao hiki kikaashiria kuwa watatu hawa hawakuwa wametengena?
Au labda ,watatu hawa wamerudiana na kuendelea na ndoa yao ya kimuziki?

cha muhimu ni kuistawisha na kuiunga mkono kazi wanayoifanya ya kuwaburudisha mafans wao!

Itazame audio  Hapa .

Share:

Wednesday 4 May 2016

ELANI X JOSE CHAMELEONE VIDEO ALERT

Baada ya kimya kwa muda, wanamuziki kutoka Kenya almaarufu Elani wameachia kibao kipya.

mastaa hawa wa nyumbani wameachia kibao kipya wakimshirikisha msanii Jose chameleone kutoka Uganda   kwa jina "My Darling"

My Darling ni wimbo wa kimapenzi unaoonyesha umuhimu wa kumwambia umpendaye mapenzi yako kwake.

Katika post yao kwenye YouTube,wameandika

"My Darling is a song we wrote to tell a beautiful story.we believe that love is an amazing and beautiful gift that we have to share with each other.As the most beautiful things cannot be seen or heard,or even touched. They must be felt with the heart.share this with your Darling, let them know how you feel."

Itazame video mpya

Hapa

Share:

Tuesday 3 May 2016

SHETTA KUACHIA WIMBO MPYA WIKI HII

Baada ya kimya kingi, msanii wa kutajika kutoka bongo,shetta aamua kuwachangamsha mashabiki wake kwa kibao kipya.

Star huyu wa nyimbo kama vile , nidanganye  na kerewa ft diamond platnumz, sina imani ft Rich Mavoko na nyingine nyingi amepanga kuachia kibao kwa jina NAMJUA katika Siku ya ijumaa wiki hii.

Kwa mashabiki wake wote, wakati ndo huu wa kumkumbuka!!!!

Share:

GET NOTICED

GET NOTICED
PRESENTER ALI. Powered by Blogger.

Author Details

contact us



Translate

Labels